<?xml version="1.0" encoding="utf-8"?>
<document>
<URL id="1">https://sw.globalvoices.org/2014/03/erdogan-aapa-kuifutilia-mbali-twita-nchini-uturuki/</URL><TITLE>
<s id="1.1">Erdogan Aapa "Kuifutilia Mbali" Twita Nchini Uturuki</s></TITLE>
<s id="1.2">Serikali ya Uturuki imeufunga mtandao wa Twita -sambamba na huduma ya Google iitwayo DNS, iliyokuwa inatumika kama njia ya mzunguko kufuatia kufungwa kwa mtandao wa twita.</s>
  
<s id="1.3">Inaonekana, hata hivyo, kuwa mpango wa serikali hiyo wa kudhibiti raia wa nchi hiyo kuwasiliana unakumbana na mipango kinzani, kwa kuwa twiti zinazotoka nchini Uturuki ndio kwanza zimeongezeka.</s><P id="1">
<s id="2.1">Kufungiwa kwa mtandao wa Twita, kulikoripotiwa kuathiri watu zaidi ya milioni 10 wanaotumia mtandao huo nchini Uturuki, hali iliyofuatia kuchapishwa kwa nyaraka zinazosemekana 'kufunua' ufisadi wa maswahiba wa karibu wa Waziri Mkuu Recep Tayyip Erdogan.</s></P><P id="2">
<s id="3.1">Taarifa za habari zinasema kuwa Erdogan ameahidi "kuufutilia mbali mtandao wa Twita" akiongeza kuwa kamwe hajali kile ambacho kingesemwa na jumuiya ya kimataifa.</s></P><P id="3">
<s id="4.1">Juan Cole anaelezea jaribio la Erdogan la kufungia huduma hiyo ya kijamii akiita "upuuzi":</s><QUOTE>
<s id="4.2">Jaribio la kipuuzi la Erdogan la kujaribu kudhibiti matumizi ya mtandao wa intaneti limekwama na kushindwa mara moja.</s>
      
<s id="4.3">Vijana wa Kituruki wana weledi kuhusiana na matumizi ya zana za kupata huduma hiyo ziitwazo Tor na VPN, na watumiaji wa Twita nchini Uturuki walijipanga haraka sana kiasi ambacho huenda kilimchanganya kichwa ndugu Erdogan.</s></QUOTE>
<s id="4.4">Erik Meyersson anaongeza:</s><QUOTE>
<s id="4.5">Watumiaji wa mtandao wa Twita nchini Uturuki walimgundua @torproject mwaka jana, haishangazi watu bado wanatwiti pamoja na kufungiwa kwa mtandao huo nchini Uturuki</s></QUOTE>
<s id="4.6">Na mtafiti wa Uturuki Zeynep Tufekci anatabasamu muda wote amvao watumiaji wa mtandao wa twita nchini Uturuki wanapaza sauti zao pamoja na kufungiwa kwa mtandao huo:</s><QUOTE>
<s id="4.7">Ingawa mtandao umefungiwa bado twiti milioni 1.2 zimeendelea kutumwa nchini Uturuki</s></QUOTE>
<s id="4.8">Hata hivyo, anaongeza:</s><QUOTE>
<s id="4.9">Kufungiwa kwa DNS, ikifuatiwa na kufungiwa kwa IPS, nani ajuaye nini kinafuata.</s>
      
<s id="4.10">Uturuki iko mbioni kuwa na weledi wa hali ya juu wa masuala ya kiteknoloji.</s>
      
<s id="4.11">Kinachofuta ni mradi wa Tor</s></QUOTE>
<s id="4.12">Kutoka Uturuki, Engin Onder anaeleza namna watumiaji wa Twita walivyosambaza ujumbe wa namna ya "kuuzunguka" ufungiaji huo:</s><QUOTE>
<s id="4.13">Mtandao wa twita umefungiwa leo nchini Uturuki, jamaa wanatengeneza huduma ya DSN ya google kwenye mabango ya chama tawala</s></QUOTE>
<AUTHOR name="Amira Al Hussaini" />
    
<TRANSLATOR name="Christian Bwaya" /></P>
</document>
<?xml version="1.0" encoding="utf-8"?>
<document>
<URL id="1">https://sw.globalvoices.org/2013/10/yemeni-bundi-atua-nje-ya-dirisha-langu/</URL><TITLE>
<s id="1.1">Yemeni: Bundi Atua Nje ya Dirisha Langu</s></TITLE>
<s id="1.2">Mwanablogu wa Yemeni, Abdulkader Alguneid amkuta bundi nje ya dirisha lake:</s><P id="1">
<s id="2.1">Kupitia mtandao wa Twita, anaelezea tukio hilo ambalo ni nadra sana kutokea:</s><QUOTE type="twitter"><P id="2">
<s id="3.1">بومة كبيرة خلف زجاج نافذتي، 1.30 بعد منتصف الليل.          Alikuwa Bundi mkubwa, nyuma ya dirisha langu la kioo, majira ya saa 7.30 usiku, tarehe pic.twitter.com/19WjfUelQ0 — abdulkader alguneid (@alguneid) 30 Octoba, 2013</s></P>
    </QUOTE>
<AUTHOR name="Amira Al Hussaini" />
    
<TRANSLATOR name="Albert Kissima" /></P>
</document>
<?xml version="1.0" encoding="utf-8"?>
<document>
<URL id="1">https://sw.globalvoices.org/2009/03/gumzo-la-moja-kwa-moja-kuhusu-virusi-vya-ukimwi-na-ukimwi-mtandaoni-tarehe-6-machi/</URL><TITLE>
<s id="1.1">Gumzo la moja kwa moja kuhusu Virusi vya ukimwi na Ukimwi mtandaoni Tarehe 6 machi</s></TITLE><P id="1">
<s id="2.1">Mradi wa Rising Voices na Global Voices wanaandaa gumzo la moja kwa moja mtandaoni kwa wanablogu na wanaharakati siku ya Ijumaa mwezi wa tatu mwaka huu(saa 11 jioni kwa saa za Nairobi) mada kuu ikiwa jinsi ya kublogu na kuongeza uelewa na habari kuhusu virusi vya ukimwi na Ukimwi.</s></P><P id="2">
<s id="3.1">Kila mmoja anakaribishwa</s></P><P id="3">
<s id="4.1">Muda:New York 3 asubuhi | Buenos Aires 6mchana | London 8mchana | Johannesburg,Beirut 10jioni | Nairobi, Moscow 11 jioni | New Delhi 1:30 usiku | Hong Kong 4usiku | Tokyo 5 usiku</s></P><P id="4">
<s id="5.1">Chumba cha gumzo:http://www.worknets.org/chat/</s><QUOTE>
<s id="5.2">Jinsi ya kujiunga:Bonyeza kingo hapo juu tumia jina lako.Kisha chagua chumba utakacho kujiunga kwa kubonyeza ingia.Baada ya kuingia chagua ukubwa wa maandishi upande wa kushoto wa kiwambo cha tarakishi yako, jiunge katika gumzo</s></QUOTE>
<s id="5.3">Gumzo la tarehe 6 mwezi wa 3 litajenga mada iliyoletwa katika majadiliano yaliofanikiwa wiki iliyopita.</s>
    
<s id="5.4">Gumzo la tarehe 27 mwezi wa pili lilitoa tamko kama vile umuhimu wa kublogu kwa watu walioathirika na virusi vya ukimwi na jukumu katika upelekaji na ushawishi wa maarifa,lakini kikubwa lililenga kwenye muongozo wa kublogu vyema ,muongozo ulitengenezwa na Global Voices kutoa ushauri tunu jinsi ya kublogu kuhusu masuala ya Virusi vya Ukimwi na Ukimwi.</s>
    
<s id="5.5">Muongozo huo bado ni kazi inayooendelea, kwa hiyo tunatafuta msaada kutengeneza na kutoa matokeo.</s>
    
<s id="5.6">Kwa wale waliokuwa na nia au waliokwisha blogu kuhusu maafa wanahimizwa kushiriki katika gumzo wiki hii, hasa wale wanaoishi au walioathirika na virusi vya ukimwi.</s>
    
<s id="5.7">Gumzo la Ijumaa litalenga masuala kama vile uanzishwaji makundi maalum ya kazi au vitengo kwa ajili ya mchakato wa kutengeneza muongozo wa kublogu vyema kadhalika gumzo hilo litajadili kuhusu aya na na mada zipi zijumuishwe kwenye muongozo.</s></P><P id="5">
<s id="6.1">Pia kuna mada nyingine ambazo utataka kujadili wakati wa gumzo,tafadhali weka maoni chini.Natumaini mtashirikiana nasi tarehe 6 mwezi wa tatu</s>
    
<AUTHOR name="Juhie Bhatia" />
    
<TRANSLATOR name="Egidio Ndabagoye" /></P>
</document>
<?xml version="1.0" encoding="utf-8"?>
<document>
<URL id="1">https://sw.globalvoices.org/2015/05/ngono-dini-na-siasa-vinapokutana-kwenye-onesho-la-sidiria-ya-kimalaya/</URL><TITLE>
<s id="1.1">Ngono, Dini na Siasa Vinapokutana Kwenye Onesho la 'Sidiria ya Kimalaya'</s></TITLE>
<s id="1.2">Mwandishi wa michezo ya kuigiza Aizzah Fatima aliigiza uhusika anaouita "mwanaharakati haki za wanawake anayevaa hijabi."</s>
  
<s id="1.3">Picha: Haki miliki ya Aizzah Fatima.</s>
  
<s id="1.4">Imechapishwa kwa ruhusa ya PRI</s><P id="1">
<s id="2.1">Makala haya na taarifa ya redio iliyoandikwa na Joyce Hackel kwa ajili ya kipindi cha redio kiitwacho The World kilichoonekana kwanza kwenye tovuti ya PRI.org mnamo Mei 28, 2015, na kimechapishwa hapa kama sehemu ya makubaliano ya ushirikiano wa kimaudhui.</s></P><P id="2">
<s id="3.1">Aizzah Fatima amekuwa akiogopa kwamba jina la igizo lake linalochezwa na mhusika mmoja, "Dirty Paki Lingerie," (Vazi lisilofaa kuvaliwa hadharani), lingeweza kuwaudhi ndugu zake wa-Asia ya Kusini.</s>
    
<s id="3.2">Lakini baada ya takribani miaka mitano ya kuigiza akiwa Toronto na baadae Turkmenistan, mwigizaji huyo Mmarekani mwenye asili ya Pakistani hajali kama jina hilo linaleta karaha.</s></P>
<P id="3" /><P id="4">
<s id="5.1">Listen to this story on PRI.org »</s></P><P id="5">
<s id="6.1">"Ilikuwa ni changamoto kubwa nilipoanza kuigiza onesho hili kupata ushirikiano wa jamii ya Waislamu wa Kimarekani," anasema.</s>
    
<s id="6.2">"Mambo yamebadilika sana."</s></P><P id="6">
<s id="7.1">Lengo hasa kwenye igizo hilo ni kusaili masuala ya kujitambua, ujinsia na dini kwa mtaamo wa Wamerekani sita wenye asili ya Kipakistani.</s>
    
<s id="7.2">Katika majuma ya hivi karibuni, Fatima na mwongozaji wake Erica Gould wamepanua kazi zao mpaka Luton, Bradford, Glasgow na London ambako wanawashirikisha Waislamu wa maeneo hayo kwenye majadiliano kupitia "mazungumzo ya mrejesho" baada ya onesho.</s></P><P id="7">
<s id="8.1">"Nimewahi kukutana na matukio ya baadhi ya kumbi za maonesho kuomba nikaoneshe onesho langu kwao, na baadae kuniarifu kwamba wameghairi kwa sababu ya woga," anasema.</s>
    
<s id="8.2">"Kuna wakati tulikuwa Bradford, ninakodhani ni moja wapo ya miji masikini zaidi na yenye watu wengi zaidi wenye asili ya pakistani nchini Uingereza, na kulikuwa na watu kwenye hadhira yangu waliokerwa na onesho hilo.</s>
    
<s id="8.3">Na walisema wazi wazi, na bado alikuja."</s></P><P id="8">
<s id="9.1">Neno "Paki" ni tusi nchini Uingereza, ambako lilitumika awali kwenye magazeti miaka ya 1960 kuwatambulisha Waasia Kusini, ikiwa ni pamoja na Wahindi, waafghani na Wabangladeshi.</s></P><P id="9">
<s id="10.1">Fatima anasema aliamua kuanza kuandika onesho hilo kujaribu kuonesha mtazamo usiozoeleka wa maisha halisi ya Wamarekani wenye asili ya Pakistani wanaoishi Marekani, na kwa sababu alikuwa ameumizwa kihisia kuambiwa kwamba hakuwa anafaa kuvaa uhusika wa waigiziji wa ki-Islamu wenye asili ya Asia Kusini.</s></P><P id="10">
<s id="11.1">"Kuna mtazamo wa kibinadamu kwenye uzoefu huu wa kuwa mwanamke wa Kiislamu (tena) Mmarekani aliyekuwa anakosekana kwenye vyombo vya habari, aliyekosekana kabisa miongoni mwa wahusika tunaowaona kwenye filamu, runinga, kumbi za maonesho," anasema.</s>
    
<s id="11.2">"Nilitaka kumwonesha mwanamke wa Kiislamu, hususani wanawake wanaofunika nywele zao, kwa namna ninavyowafahamu, wanaharakati na watetezi wa haki za wanawake na wapaza sauti wakubwa wa kushinikiza mambo."</s></P><P id="11">
<s id="12.1">Fatima anasema mtazamo hasi na wa jumla kwa Waasia wa Kusini utakoma katika miongo ijayo.</s></P><P id="12">
<s id="13.1">"Ninatumaini kwenye maisha yangu, miaka 30 ijayo, tutaweza kutazama nyuma kuona nyakati hizi na kusema, 'Tumevuka kipindi hicho," anasema.</s>
    
<s id="13.2">"Tumepiga hatua."</s>