<?xml version="1.0" encoding="utf-8"?> <document> <URL id="1">https://sw.globalvoices.org/2014/03/global-voices-yaanzisha-ushirikiano-na-shirika-la-kukutanisha-wakimbizi/</URL><TITLE> <s id="1.1">Global Voices Yaanzisha Ushirikiano na Shirika la Kukutanisha Wakimbizi</s></TITLE> <s id="1.2">Wakimbizi Wakutanishwa Hivi sasa dunia imeunganishwa zaidi kuliko ilivyowahi kuwa kabla, lakini wakati maelfu ya wakimbizi wanazikimbia nchi zao zenye migogoro au majanga na hivyo kupoteza mawasiliano na ndugu na jamaa zao -ambao mara nyingi hupoteza mawasiliano hayo milele.</s> <s id="1.3">Katika wakimbizi 43 duniani kote, wengi wao wanasemekana hawaweza tena kuonana na familia zao tena kwa sababu tu ya kukosa namna ya kuwasiliana nao.</s><P id="1"> <s id="2.1">Refugees United ni shirika ambalo hutumia mtandao wa intaneti na simu za kiganjani kusaidia familia zilizopoteana.</s> <s id="2.2">Watumiaji wa mfumo wao huweka taarifa zao binafsi wanazoona ni salama kuzitangaza hadharani ambazo bado ziwafanye wabaki kuwa na faragha ya kutokufahamika.</s> <s id="2.3">Watu wengi tayari wameshakutana na familia na marafiki zao kupitia mfumo huu wa Shirika la Wakimbizi Wakutana, lakini kuendelea kwa mafanikio hayo kutategemea ni jinsi gani wakimbizi watajua kuwa kuna kitu kama hicho.</s></P><P id="2"> <s id="3.1">Watafikiwaje?</s></P><P id="3"> <s id="4.1">Tangu mwaka uliopita, watafsiri wa Global Voices wamekuwa wakifanya kazi na shirika hilo la kukutanisha wakimbizi kwa kutafsiri vitendea kazi vyao, kutumia mitandao ya kijamii na ujumbe mfupi wa meneno (SMS) kwenda katika lugha za Kiswahili, Kifaransa, Kisomali, Kiamhari, Kiarabu cha Sudani na Kiarabu asilia.</s> <s id="4.2">Tumeshirikiana nao kuwapa ushauri mahsusi kwa maeneo yanayolengwa kuhusu namna ya kutunga ujumbe unaoeleweka na unaokubalika kiutamaduni.</s></P><P id="4"> <s id="5.1">Shirika la Refugees United linasema linalenga kufikia watu milioni 1 ifikapo mwaka 2015 na Global Voices inajisikia fahari kutoa ushirikiano wa karibu.</s></P><P id="5"> <s id="6.1">"Ushirikiano na Global Voices ni ushahidi wa namna tunavyoweza kuzifikia familia nyingi zaidi kwa kushirikiana na mtandao wao imara wa watafsiri na wanablogu,” anasema Ida Jeng wa shirika hilo la Refugees United.</s></P><P id="6"> <s id="7.1">Nguvu ya kuungana kwa mara nyingine</s></P><P id="7"> <s id="8.1">Kwenye blogu ya Refugees United kuna masimulizi yasiyohesabika kuhusu miradi ya kuwafikia watu na namna watu waliopoteana walifanikiwa kukutana kwa mara nyingine.</s></P><P id="8"> <s id="9.1">Video hii inaelezaea simulizi la mwanamke aitwaye Estelle aliyekutana na dada yake baada ya kutengana naye kwa miaka 16.</s></P><P id="9"> <s id="10.1">Na video hii inawaonyesha kaka wawili wa ki-Kongo waliotengana kwa miaka 15 na hatimaye kukutana kwa mara ya kwanza kwenye zana ya mtandaoni ya Google Hangout on Air baada ya kufahamishana mahali walipo kupitia mtandao wa shirika la Refugees United.</s> <AUTHOR name="Solana Larsen" /> <TRANSLATOR name="Christian Bwaya" /></P> </document> <?xml version="1.0" encoding="utf-8"?> <document> <URL id="1">https://sw.globalvoices.org/2014/04/23/</URL> <TITLE id="2">Habari za uandishi wa kiraia kutoka 2014 April 23</TITLE></document> <?xml version="1.0" encoding="utf-8"?> <document> <URL id="1">https://sw.globalvoices.org/2010/04/03/</URL> <TITLE id="2">Habari za uandishi wa kiraia kutoka 2010 April 03</TITLE></document> <?xml version="1.0" encoding="utf-8"?> <document> <URL id="1">https://sw.globalvoices.org/2009/10/misri-watawala-wa-kiimla-na-wake-zao/</URL><TITLE> <s id="1.1">Misri: Watawala Wa Kiimla na Wake Zao</s></TITLE> <s id="1.2">Baada ya kuziangalia picha za mke wa Rais wa Cameroon, Mmisri Zeinobia anasema: “Sijui ni ni kiasi gani cha pesa alichotumia kwa ajili ya nywele zake na muonekano wake lakini ninafahamu kuwa watu wa Camerron wanazihitaji zaidi hizo pesa.”</s> <AUTHOR name="Amira Al Hussaini" /> <TRANSLATOR name="j nambiza tungaraza" /></document> <?xml version="1.0" encoding="utf-8"?> <document> <URL id="1">https://sw.globalvoices.org/2014/08/hali-ya-kusikitisha-katika-kituo-cha-magarimoshi-cha-mumbai/</URL><TITLE> <s id="1.1">Hali ya Kusikitisha Katika Kituo cha Magarimoshi cha Mumbai</s></TITLE> <s id="1.2">Mwanablogu Antarik Anwesan anaelezea hali halisi ya kile kinachoendelea katika kituo cha magarimoshi cha Goregaon kilichopo Mumbai, India.</s> <s id="1.3">Gari moshi lifanyalo safari za ndani liliondoka kituoni bila ya kutoa taarifa wakati abiria walipokuwa wakiharakisha kuingia.</s> <s id="1.4">Kadri ya garimoshi lilivyoongeza mwendo, watu wawili walianguka kupitia mlangoni, chupuchupu kupoteza maisha.</s> <s id="1.5">Taarifa ya tukio hili haikuripotiwa katika kituo chochote cha habari.</s> <s id="1.6">Mwanablogu huyu afafanua kuwa, pamoja na kuwa waathirika katika magarimoshi yafanyayo safari za ndani huongezeka kila mwaka, serikali haijaweza kuweka mikakati ya usalama wa usafiri wa magarimoshi unaotumiwa na watu wengi zaidi.</s> <AUTHOR name="Rezwan" /> <TRANSLATOR name="Albert Kissima" /></document> <?xml version="1.0" encoding="utf-8"?> <document> <URL id="1">https://sw.globalvoices.org/2008/08/angola-brazil-mshituko-na-utengano-wa-kitamaduni/</URL><TITLE> <s id="1.1">Angola, Brazil: Mshituko na Utengano wa Kitamaduni</s></TITLE><P id="1"> <s id="2.1">Kinyago cha mtumwa mweusi kilichochongwa na Luiz Paulino da Cunha.</s> <s id="2.2">Picha kwa hisani ya Asasi ya Watoto Walio Hatarini.</s></P><P id="2"> <s id="3.1">Angola na Brazil zina uhusiano maalum baina yao, kutokana na matumizi ya lugha moja na pamoja na historia yao ya kutawaliwa huko nyuma - nchi hizi mbili zilikuwa sehemu ya himaya ya Wareno – na utamaduni wa pamoja unaotoka na historia ya asili moja.</s> <s id="3.2">Tangu mwaka 2000, biashara kati ya mataifa haya mawili ilianza kukuwa na sasa inachanua.</s> <s id="3.3">Kwa mujibu wa Chama cha Makampuni ya KiBrazili nchini Angola (AEBRAN), biashara kati ya mataifa mawili haya imekuwa kwa mara sita zaidi tangu mwaka 2002.</s></P><P id="3"> <s id="4.1">Kutokana na kuongezeka huko kwa biashara, uwepo wa makampuni ya Brazili nchini Angola pia kumeongezeka.</s> <s id="4.2">Kumepelekea, pia ongezeko la uhamiaji kutoka Brazili kwenda Angola kwa kadri ya asilimia 70 kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita.</s> <s id="4.3">Inakadiriwa kuwa kuna Wabrazili 5,000 waliosajiliwa nchini Angola haswa wanaojishughulisha na masuala ya ujenzi, uchimbaji madini na biashara za mazao ya kilimo.</s> <s id="4.4">Maendeleo haya mapya katika historia ya Angola, nchi iliyozoea kuwa na uhamiaji kuelekea ng'ambo nyingine ya Atlantiki, yanapelekea kwenye mtikisiko wa kiutamaduni usioweza kuepukika kwa wote, Wabrazili na Waangola pia.</s></P><P id="4"> <s id="5.1">Hapa chini kuna habari zilizopachikwa katika kurasa za blogu mbili zikionyesha mitazamo tofauti baina ya watu wawili kwa kuibua masuala muhimu kama uhamiaji, ubaguzi wa rangi, ukabila na heshima miongoni mwa watu.</s> <s id="5.2">Zaidi ya yote, wanabainisha mahusiano ya namna mbalimbali na yenye mchanganyiko - kwa kuwianisha yale yanayofanana na yanayotofautiana - miongoni mwa watoto hao waliotenganishwa na bahari wakati wa makuzi yao.</s></P> <P id="5" /><P id="6"> <s id="7.1">Kinyago cha mtumwa mweusi kilichochongwa na Luiz Paulino da Cunha.</s> <s id="7.2">Picha kwa hisani ya Asasi ya Watoto Walio Hatarini.</s></P><P id="7"> <s id="8.1">Migas , Mbrazili anayeishi Luanda, anasema yafuatayo:</s><QUOTE> <s id="8.2">Nimekuwa nikiuangalia uchaguzi wa Septemba kwa mtazamo chanya.</s> <s id="8.3">Nina matumaini kwamba matukio ya vurumai yaliyowahi kutokea huko nyuma hayatatokea tena.</s> <s id="8.4">Kila mmoja anakubaliana kuwa taifa linahitaji amani ili kuweza kufuatilia makuzi ya uchumi, maendeleo, hali bora ya maisha.</s> <s id="8.5">Labda maisha bora ni lengo lililokwishasahaulika.</s> <s id="8.6">Hata hivyo, tukio linakaribia.</s>